Tunaamini kauli huru, haki ya kujieleza, na haki ya kusikiliza. Tunaamini haki ya upatikanaji wa zana za mawasiliano na habari kwa watu wote.
Kufanikisha hayo, tunaazimia kumwezesha kila anayetaka kujieleza awe na njia za kujieleza, na kwa kila anayetaka kusikiliza awe na njia za kusikiliza.
Kutokana na faida za zana mpya za mawasiliano na habari, kujieleza hakutawaliwi tena na wanaomiliki njia za uchapishaji na usambazaji, au serikali zinazozuia uhuru wa fikra na mawasiliano. Hivi sasa kila mmoja anaweza kuwa na nguvu za vyombo vya habari. Kila mmoja ana uwezo wa kuelezea simulizi zake kwa dunia nzima.
Tunaazimia kujenga maelewano penye utengano ili tuweze kufahamiana kwa undani zaidi. Tunaazimia kufanya kazi pamoja kwa ufanisi na kuchukua hatua kwa nguvu zaidi.
Tunaamini nguvu za mahusiano ya moja kwa moja. Udugu kati ya watu toka tamaduni mbalimbali ni wa karibu, kisiasa, na wenye nguvu. Tunaamini majadiliano bila kujali tofauti zetu ni muhimu kwa ajili ya dunia ya kesho ambayo ni huru, ya haki, ustawi na endelevu…kwa wananchi wote wa sayari hii.
Wakati tukiendelea kufanya kazi na kuongea kama watu binafsi, tunaazimia kutambua na kuendeleza maslahi na malengo yetu ya pamoja. Tunaahidi kuheshimu, kusaidia, kufundisha, kujifunza, na kusikilizana.
Sisi ni Sauti za Dunia.





























Steve SharraLatest of 12 posts
Francois Bacha and Marie-Josée RizkallahLatest of 2 posts
Alan DavidsonLatest of 1 posts
Nishadha SilvaLatest of 3 posts
Lasto AdriLatest of 19 posts
Moussa BashirLatest of 179 posts
Maya NortonLatest of 49 posts
John LiebhardtLatest of 17 posts
SudaneseDrimaLatest of 20 posts
Sinisa BoljanovicLatest of 15 posts
Solana LarsenLatest of 28 posts
Salam AdilLatest of 98 posts